07/07/2021
HADITHI: CHOZI LA MNYONGE
MTUNZI: Mwaki Ze Done.
MWANDISHI:Mwaki Ze Done.
Sehemu ya 2.
Baada ya askari kuniambia makosa yote yanayonikabili nilish*tuka na kudondoka chini baada ya hapo sikuelewa kilichoendelea.
Nilikuja kuzinduka nikiwa nipo hospitalini na pingu mkononi na nilianza kukumbuka nini kilitokea, ndipo nikakumbuka yale maongezi ya mara ya mwisho na afande ambayo yalikuwa hivi
"Ndiyo ni 3 siyo 4"
"Ni yapi hayo??"
"La kwanza unatuhumiwa kwa mauaji, lapili ni ubakaji na latatu ni wizi kwa kutumia siraha za moto"
"Mungu wangu!!! Mimi nimeua??"Nilish*tuka kwa kutajiwa yale makosa nikiwa siamini.
"Ndiyo umeua na ushahidi upo"
"Afande mimi katika maisha yangu sijawahi kuua wala kuiba cha mtu japo Mimi na wazazi wangu ni maskini"
"Ndo k**a ulivyo sikia k**a nawe una ushahidi wa kukanusha makosa yako tueleze??"
"Kwanza afande bado sielewi, nimemuua nani?? Na nimemubaka nani?? Na nimeiba wapi hapo ndio ntajua ushahidi wa kujitetea natoa vipi" nilimwambia yule afande machozi yakiwa yananitoka
"Kwanza umemubaka mtoto wa mama mwenye nyumba, pili uliwatishia wapangaji wenzako na siraha na kuwachukulia vitu vyao, kosa kubwa kabisa ambalo ndo nakusikitia umewaua wazazi wako wote wawili kwa kuwakatakata na mapanga na ushahidi upo"
"Niniiiiii baba na mama wameuawa??" Niliuliza kwa jasiba kwa muda huo nilikuwa nimemukunja yule afande shati lake
"Ndiyo wameuawa na muuaji mkuu ni wewe" Baada ya kuambiwa ivo nilianza kuhisi kizunguzungu na kudondoka.
"Eheee vipi we gaidi umeamuka nilijua Mungu atakuchukua moja kwa moja??" Nilish*tushwa na Doctor nikiwa bado nakumbuka na kutafakari zile tuhuma nilizo ambiwa na afande katika chumba cha mahojiano.
"Doctor mimi siyo gaidi"
"Bana me siyo hakimu wa kunieleza mi ninachojua na nilichoambiwa ni kwamba niwe makini na wewe kwasababu ni mtu hatari na hapo nje kuna askari wa nne kwa ajili ya ulinzi tuu"
Nilishangaa maneno ya Doctor kila kitu niliona ni k**a ndoto ila ndio ulikuwa uhalisia wenyewe, baada ya Doctor kuondoka nilikumbuka habari za wazazi wangu kufa nilianza kupiga kelele mule wodini mpaka maaskari waliokuwa nje waliingia ndani
"Eheee unataka kufanya tena matukio eeeeee??" Aliongea askari mmoja baada ya kuingia ndani
"Afande me sina makosa niacheni nikawaangalie wazazi wangu kijijini kwetu k**a kweli wamekufa" niliongea huku nikiwa nalia k**a mtu aliyechizika
"We umechanganyikiwa eee?? Kwani Doctor hajakwambi??"
Nilitahamaki na swali la askari nilitulinza munkari kidogo na kuuliza
"Hajanambia!!!? Kuhusu nini??"
"Doctor hajakwambi kwamba wazazi wako tayari wameshazikwa??"
"Wamezikwa!!!?? Lini?? " Niliuliza huku nikiwa sielewi askari kitu anachoongea
"Ndiyo wamezikwa, unajua mara baada ya wewe kuzimia kule kituoni ni muda gani umepita mpaka wewe kuja kuzinduka hii leo??"
Nilikaaa kimya huku nikiwa sielewi kila kitu ambacho askari anaongea yaani kila kitu niliona ni k**a tunataniana tuu.
"Unaka kimya eeee?? Ila ndo ujue hivyo hapa hospitali umekaa wiki moja na toka wiki iliyopita ndo umezinduka leo na wazazi wako walizikwa na serikali baada ya ndugu kukosekana"aliongea yule askari na kutoka nje na kuniacha nikiwa nipo kimya ndani. Nilijikuta machozi yanaanza kunitoka tena na nilikumbuka jinsi maisha ya wazazi wangu yalivyo kuwa kijijini na jinsi walivyoniasa kutokuja mjini niliona huuu ndo mwisho wa dunia ambao huwa unazungumziwa. Siku hiyo ilikuwa ni kulia tuu mpaka saa tatu usiku nilikuwa nalia na nilikuwa sijaona mtu yeyote akiingia chumbani kwangu nilipolazwa hata wa kuniletea chakula hakuwepo. Ilifika asubuhi nikiwa sijala kitu chochote na mwili ulikuwa hauna nguvu kabisa, Mara aliingia nesi mmoja akiwa anakuja kwa kunyata huku kabeba chupa ya uji.
"Chukua huu uji kunywa haraka haraka maana tumeambiwa usipewe chakula chochote mpaka kesho ambapo ndo siku ya kwenda mahak**ani" aliongea yule nesi huku akiwa makini asije akash*tukiwa.
Kwakuwa nilikuwa na njaa sana sikutaka kuuliza chochote mpaka nishibe, nilichukua ile chupa nilianza kunywa uji bila hata kumiminia kwenye kikombe wala kujali ni wa moto, yule nesi aliniangalia kwa huruma na kuniuliza
"Hivi ni kweli kaka wewe ndio umefanya yote hayo??"
"Dada mi sijui chochote yawezekana ni kweli au so kweli"
"Mi nikikwangalia kabisa usoni naona siyo wewe, ila kinachoniuma unaenda kufia gerezani"
"Dada k**a ni ivo itakuwa bora zaidi "
"Haya bana mi naondoka ila usimwambie mtu k**a kuna mtu aliingia humu ndani" Yule nesi aliniambia na kutoka nje, ile tuu ndo anataka kufungua mlango alikutana uso kwa macho na mkuu wa kituo cha polisi akiwa na Doctor mkuu wa hospitali, nilimuona yule nesi anatetemeka mpaka chupa aliyokuwa ameificha ili mudondoka.
Je nini kitatokea kwa pendo??
Je itakuwaje kwa kijana jeriko??
Itaendelea.....
Usikose sehemu ya 3
Ili kuisoma hadithi hii chapu kwa haraka tembelea page ya *Mwaki Ze Done Story* au jiunge na group la facebook *hadithi za Mwaki Ze Done*
Contact: 0742138331