DJ martin kenya

DJ martin kenya Worship God in splendor of holiness

12/02/2025

Yuda 1:5-13
[5]Tena napenda kuwakumbusha, ijapokuwa mmekwisha kujua haya yote, ya kwamba Bwana, akiisha kuwaokoa watu katika nchi ya Misri, aliwaangamiza baadaye wale wasioamini.
[6]Na malaika wasioilinda enzi yao wenyewe, lakini wakayaacha makao yao yaliyowahusu, amewaweka katika vifungo vya milele chini ya giza kwa hukumu ya siku ile kuu.
[7]K**a vile Sodoma na Gomora na miji iliyokuwa kando-kando, waliofuata uasherati kwa jinsi moja na hawa, wakaenda kufuata mambo ya mwili yasiyo ya asili, imewekwa kuwa dalili, wakiadhibiwa katika moto wa milele.
[8]Kadhalika na hawa, katika kuota kwao, huutia mwili uchafu, hukataa kutawaliwa, na kuyatukana matukufu.
[9]Lakini Mikaeli, malaika mkuu, aliposhindana na Ibilisi, na kuhojiana naye kwa ajili ya mwili wa Musa, hakuthubutu kumsh*taki kwa kumlaumu, bali alisema, Bwana na akukemee.
[10]Lakini watu hawa huyatukana mambo wasiyoyajua, na mambo wayatambuayo kwa asili wajiharibu kwayo k**a wanyama wasio na akili.
[11]Ole wao! Kwa sababu walikwenda katika njia ya Kaini, na kulifuata kosa la Balaamu pasipo kujizuia, kwa ajili ya ujira, nao wameangamia katika maasi ya Kora.
[12]Watu hawa ni miamba yenye hatari katika karamu zenu za upendo walapo karamu pamoja nanyi, wakijilisha pasipo hofu; ni mawingu yasiyo na maji, yachukuliwayo na upepo; ni miti iliyopukutika, isiyo na matunda, iliyokufa mara mbili, na kung’olewa kabisa;
[13]ni mawimbi ya bahari yasiyozuilika, yakitoa aibu yao wenyewe k**a povu; ni nyota zipoteazo, ambao weusi wa giza ndio akiba yao waliowekewa milele.

11/02/2025

Zaburi 24:1-10
[1]Nchi na vyote viijazavyo ni mali ya BWANA,
Dunia na wote wakaao ndani yake.
(A Psalm of David.) The earth is the LORD'S, and the fulness thereof; the world, and they that dwell therein.
[2]Maana ameiweka misingi yake juu ya bahari,
Na juu ya mito ya maji aliithibitisha.
For he hath founded it upon the seas, and established it upon the floods.
[3]Ni nani atakayepanda katika mlima wa BWANA?
Ni nani atakayesimama katika patakatifu pake?
Who shall ascend into the hill of the LORD? or who shall stand in his holy place?
[4]Mtu aliye na mikono safi na moyo mweupe,
Asiyeiinua nafsi yake kwa ubatili,
Wala hakuapa kwa hila.
He that hath clean hands, and a pure heart; who hath not lifted up his soul unto vanity, nor sworn deceitfully.
[5]Atapokea baraka kwa BWANA,
Na haki kwa Mungu wa wokovu wake.
He shall receive the blessing from the LORD, and righteousness from the God of his salvation.
[6]Hiki ndicho kizazi cha wamtafutao,
Wakutafutao uso wako, Ee Mungu wa Yakobo.
This is the generation of them that seek him, that seek thy face, O Jacob. Selah.
[7]Inueni vichwa vyenu, enyi malango,
Inukeni, enyi malango ya milele,
Mfalme wa utukufu apate kuingia.
Lift up your heads, O ye gates; and be ye lift up, ye everlasting doors; and the King of glory shall come in.
[8]Ni nani Mfalme wa utukufu?
BWANA mwenye nguvu, hodari,
BWANA hodari wa vita.
Who is this King of glory? The LORD strong and mighty, the LORD mighty in battle.
[9]Inueni vichwa vyenu, enyi malango,
Naam, viinueni, enyi malango ya milele,
Mfalme wa utukufu apate kuingia.
Lift up your heads, O ye gates; even lift them up, ye everlasting doors; and the King of glory shall come in.
[10]Ni nani huyu Mfalme wa utukufu?
BWANA wa majeshi,
Yeye ndiye Mfalme wa utukufu.
Who is this King of glory? The LORD of hosts, he is the King of glory. Selah.

08/02/2025

Matthew 18:8-9
And if your hand or your foot causes you to sin, cut it off and throw it away. It is better for you to enter life crippled or lame than with two hands or two feet to be thrown into the eternal fire. And if your eye causes you to sin, tear it out and throw it away. It is better for you to enter life with one eye than with two eyes to be thrown into the hell of fire.

07/02/2025

1 Yohana 2:18-22
[22]Ni nani aliye mwongo ila yeye akanaye ya kuwa Yesu ni Kristo? Huyo ndiye mpinga Kristo, yeye amkanaye Baba na Mwana.
Who is a liar but he that denieth that Jesus is the Christ? He is antichrist, that denieth the Father and the Son.

06/02/2025

1 Wakorintho 15:34
[34]Tumieni akili k**a ipasavyo, wala msitende dhambi; kwa maana wengine hawamjui Mungu. Ninanena hayo niwafedheheshe.
Awake to righteousness, and sin not; for some have not the knowledge of God: I speak this to your shame.

05/02/2025

1 Wakorintho 15:58
[58]Basi, ndugu zangu wapendwa, mwimarike, msitikisike, mkazidi sana kutenda kazi ya Bwana sikuzote, kwa kuwa mwajua ya kwamba taabu yenu siyo bure katika Bwana.
Therefore, my beloved brethren, be ye stedfast, unmoveable, always abounding in the work of the Lord, forasmuch as ye know that your labour is not in vain in the Lord.

04/02/2025

Isaya 5:13-14
[13]Kwa sababu hiyo watu wangu wamechukuliwa mateka, kwa kukosa kuwa na maarifa; na watu wao wenye cheo wana njaa, na wengi wao waona kiu sana.
Therefore my people are gone into captivity, because they have no knowledge: and their honourable men are famished, and their multitude dried up with thirst.
[14]Kwa hiyo kuzimu kumeongeza tamaa yake, kumefunua kinywa chake bila kiasi; na utukufu wao, na wingi wao, na ghasia yao, naye pia afurahiye miongoni mwao, hushuka na kuingia humo.
Therefore hell hath enlarged herself, and opened her mouth without measure: and their glory, and their multitude, and their pomp, and he that rejoiceth, shall descend into it.

03/02/2025

Yeremia 29:14-15
[14]Nami nitaonekana kwenu, asema BWANA, nami nitawarudisha watu wenu waliofungwa, nami nitawakusanya ninyi, nikiwatoa katika mataifa yote, na katika mahali pote, nilikowafukuza, asema BWANA; nami nitawaleta tena, hata mahali ambapo kutoka hapo naliwafanya mchukuliwe mateka.
And I will be found of you, saith the LORD: and I will turn away your captivity, and I will gather you from all the nations, and from all the places whither I have driven you, saith the LORD; and I will bring you again into the place whence I caused you to be carried away captive.
[15]Maana mmesema, BWANA ametuinulia manabii huko Babeli.
Because ye have said, The LORD hath raised us up prophets in Babylon;

02/02/2025

2 Petro 2:20-22
[20]Kwa maana wale waliokwisha kuyakimbia machafu ya dunia kwa kumjua Bwana na Mwokozi Yesu Kristo, k**a wakinaswa tena na kushindwa, hali yao ya mwisho imekuwa mbaya kuliko ile ya kwanza.
For if after they have escaped the pollutions of the world through the knowledge of the Lord and Saviour Jesus Christ, they are again entangled therein, and overcome, the latter end is worse with them than the beginning.
[21]Maana ingekuwa heri kwao k**a wasingaliijua njia ya haki, kuliko kuijua, kisha kuiacha ile amri takatifu waliyopewa.
For it had been better for them not to have known the way of righteousness, than, after they have known it, to turn from the holy commandment delivered unto them.
[22]Lakini imetukia kwao sawasawa na ile mithali ya kweli, Mbwa ameyarudia matapiko yake mwenyewe, na nguruwe aliyeoshwa amerudi kugaa-gaa matopeni.
But it is happened unto them according to the true proverb, The dog is turned to his own vomit again; and the sow that was washed to her wallowing in the mire.

01/02/2025

Ezekieli 3:18-19
[18]Nimwambiapo mtu mbaya, Hakika utakufa; wewe usimpe maonyo, wala husemi na huyo mtu mbaya ili kumwonya, kusudi aache njia yake mbaya na kujiokoa roho yake; mtu yule mbaya atakufa katika uovu wake; lakini damu yake nitaitaka mkononi mwako.
When I say unto the wicked, Thou shalt surely die; and thou givest him not warning, nor speakest to warn the wicked from his wicked way, to save his life; the same wicked man shall die in his iniquity; but his blood will I require at thine hand.
[19]Lakini ukimwonya mtu mbaya, wala yeye hauachi ubaya wake, wala njia yake mbaya, atakufa katika uovu wake; bali wewe umejiokoa roho yako.
Yet if thou warn the wicked, and he turn not from his wickedness, nor from his wicked way, he shall die in his iniquity; but thou hast delivered thy soul.

31/01/2025

Zaburi 14:1-7
[1]Mpumbavu amesema moyoni, Hakuna Mungu;
Wameharibu matendo yao na kuyafanya chukizo,
Hakuna atendaye mema.
(To the chief Musician, A Psalm of David.) The fool hath said in his heart, There is no God. They are corrupt, they have done abominable works, there is none that doeth good.
[2]Toka mbinguni BWANA aliwachungulia wanadamu,
Aone k**a yuko mtu mwenye akili,
Amtafutaye Mungu.
The LORD looked down from heaven upon the children of men, to see if there were any that did understand, and seek God.
[3]Wote wamepotoka, wameoza wote pamoja,
Hakuna atendaye mema,
La! Hata mmoja.
They are all gone aside, they are all together become filthy: there is none that doeth good, no, not one.
[4]Je! Wote wafanyao maovu hawajui?
Walao watu wangu k**a walavyo mkate,
Hawamwiti BWANA.
Have all the workers of iniquity no knowledge? who eat up my people as they eat bread, and call not upon the LORD.
[5]Hapo ndipo walipoingiwa na hofu nyingi,
Maana Mungu yupo pamoja na kizazi cha haki.
There were they in great fear: for God is in the generation of the righteous.
[6]Mnalitia aibu shauri la mtu mnyonge,
Bali BWANA ndiye aliye kimbilio lake.
Ye have shamed the counsel of the poor, because the LORD is his refuge.
[7]Laiti wokovu wa Israeli utoke katika Sayuni!
BWANA awarudishapo wafungwa wa watu wake;
Yakobo atashangilia,
Israeli atafurahi.
Oh that the salvation of Israel were come out of Zion! when the LORD bringeth back the captivity of his people, Jacob shall rejoice, and Israel shall be glad.

31/01/2025

Isaya 55:9
[9]Kwa maana k**a vile mbingu zilivyo juu sana kuliko nchi, kadhalika njia zangu zi juu sana kuliko njia zenu, na mawazo yangu kuliko mawazo yenu.
For as the heavens are higher than the earth, so are my ways higher than your ways, and my thoughts than your thoughts.

30/01/2025

1 Wathesalonike 5:17
[17]ombeni bila kukoma;
Pray without ceasing.

29/01/2025

Isaya 31:1-9
[1]Ole wao watelemkao kwenda Misri wapate msaada, na kutegemea farasi; watumainio magari kwa kuwa ni mengi, na wapanda farasi kwa kuwa ni hodari sana; lakini hawamwangalii Mtakatifu wa Israeli, wala hawamtafuti BWANA!
Woe to them that go down to Egypt for help; and stay on horses, and trust in chariots, because they are many; and in horsemen, because they are very strong; but they look not unto the Holy One of Israel, neither seek the LORD!
[2]Lakini yeye naye ana akili, naye ataleta uovu, wala hatayatangua maneno yake; bali ataondoka juu ya nyumba yao watendao mabaya, na juu ya msaada wa hao watendao maovu.
Yet he also is wise, and will bring evil, and will not call back his words: but will arise against the house of the evildoers, and against the help of them that work iniquity.
[3]Basi Wamisri ni wanadamu wala si Mungu, na farasi zao ni nyama wala si roho; na BWANA atakaponyosha mkono wake, yeye asaidiaye atajikwaa, na yeye asaidiwaye ataanguka, nao wote pamoja watakoma.
Now the Egyptians are men, and not God; and their horses flesh, and not spirit. When the LORD shall stretch out his hand, both he that helpeth shall fall, and he that is holpen shall fall down, and they all shall fail together.
[4]Maana BWANA aniambia hivi, K**a vile ilivyo simba angurumapo na mwana-simba juu ya mawindo yake, wachungaji wengi wakiitwa ili kumpiga, lakini hatiwi hofu na sauti zao, wala kufanya woga kwa sababu ya mshindo wao; ndivyo BWANA wa majeshi atakavyoshuka ili kufanya vita juu ya mlima Sayuni, na juu ya kilima chake.
For thus hath the LORD spoken unto me, Like as the lion and the young lion roaring on his prey, when a multitude of shepherds is called forth against him, he will not be afraid of their voice, nor abase himself for the noise of them: so shall the LORD of hosts come down to fight for mount Zion, and for the hill thereof.
[5]K**a ndege warukao, BWANA wa majeshi ataulinda Yerusalemu; ataulinda na kuuokoa, atapita juu yake na kuuhifadhi.

27/01/2025

(A)OGOPA SANA MUNGU
Nikitafakari ukuu na matendo ya ajabu ya Bwana Mungu hutenda, waah! Ogopa sana Mungu.
Kilichompata mfalme Nebukadreza kwa kujisahau na kutaka kujipa utukufu kwa mafanikio yake. Aliona yote yamechangiwa na nguvu na uwezo wake mwenye badala ya Mungu, weeh! Ogopa sana Mungu.
Alisahau kuwa Mungu aliye juu ndiye anayemiliki katika ufalme wa wanadamu naye humpa yeye amtakaye awaye yote.Ghai! Ogopa sana Mungu.
Nebukadreza aliyefanywa kuwa k**a mnyama na makao yake yakawa pamoja na wanyama wa kondeni, akalishwa majani k**a ng'ombe. Ogopa sana Mungu. (Danieli 4:28)
Huyo ni Mungu tunayeabudu hajawai badilika.Ni mwanzo tena mwisho.
Ole wao wanaowaabudu na kutegemea wanadamu kuwa tegemea lao badala ya Jehovah Mungu.
Ole wao wanaotumia uwezo, mali au nguvu walizonazo kuwanyanyasa walio chini yao au maskini na kujiona wanaweza kuabudiwa eti hao wengine hawawezi ishi badala ya kushukuru Mungu kwa mafanikio.
Bila Mungu huwezi lolote wewe! Shukuru Mungu kwa kila jambo. Sifa na utukufu ni zake milele na siku zote.
Mafanikio yako yawe baraka kwa wengie huku sifa na utukufu ukimpa Bwana Mungu.
Tubuni na mtafute uso Bwana Mungu kupitia Yesu kristo mkombozi wa ulimwengu, maadamu anapatikana. (Isaiah 55:6)

27/01/2025

Wakolosai 1:13-14
[13]Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake;
Who hath delivered us from the power of darkness, and hath translated us into the kingdom of his dear Son:
[14]ambaye katika yeye tuna ukombozi, yaani, msamaha wa dhambi;
In whom we have redemption through his blood, even the forgiveness of sins:

Address

Kilingili
Kakamega

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when DJ martin kenya posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to DJ martin kenya:

Videos

Share